Wengi tuna mawazo na mipango mingi mizuri, ambayo
tunajua kuwa tukiitekeleza kutasonga mbele sana kimafanikio.
Lakini tunasubiri wakati muafaka, kwa kuamini kuwa
sasa mazingira kama hayaruhusu hivi.
Lakini kiukweli
wakati muafaka ni sasa. Kuna msemo wa kizungu unasema SOMETIMES LETTER BECOMES NEVER.
Huo wakati mzuri na muafaka unaousubiri unaweza
usije.
Hadi pale utakapo amua kuufanya wakati uliopo kuwa
wakati muafaka.
Mara nyingi tunaahirisha siyo kwa sababu ya wakati
bali kwa sababu ya kuogopa kuanza. Halafu tunajificha kwenye kichaka cha
wakati.
Hakuna hasara katika kutenda, maana kama ukifanikiwa
utafurahia, na kama usipo fanikiwa utajifunza .
Na mambo mengine lazima ujifunze kwanza,
HIVYO
JIFUNZE SASA.
©Grant Sumaye
+255 763 449
749
Facebook/
Grant sumaye
Instagram:
Grant_s.s

0 comments:
Post a Comment