NONDO NO. 14 – KUWA JIRANI
NA WATU WANAOKUPA SABABU YA KUENDELEA.
Siyo kila mtu
anaelekea unapoelekea wewe. Ambatana na watu wanaolekea unapo elekea wewe. Ukitumia
muda mwingi na watu ambao hapo ulipo wao ndo wameshafika, basi lazima
watakufanya na wewe uwe umeshafika.
Mbaya zaidi ni pale
unapo jaribu kung’ang’ana na watu ambao wanarudi ulipo toka. Nakuhakikishia lazima
watakurudisha nyumba.
Huwezi waepuka kabisa
watu wa aina hiyo kwenye maisha, labda kama utatafuta dunia nyingine.
Ninacho maanisha ni
kwamba, tafuta watu ambao watakupa sababu ya kuendelea hata pale unapojisikia
kusimama ama kurudi nyuma.
Tafuta watu watakao
kuvuta ukizembea
Tafuta watu watakao
kutia moyo ukikata tama.
Watakao kuhamasisha
ukilegea moyo,
Watakao kukumbusha
ukisahau.
Watafute watu wa
namna hiyo na utumia muda wako mwingi zaidi kuwa nao kuliko lile kundi la
kwanza.

0 comments:
Post a Comment