1 NONDO YA 12. UNAWEZA KUFANYA KARIBU KILA KITU
Kuna
watu watakufa wakiwa masikini kwa sababu wanaona hakuna kitu wanachoweza
kufanya kikawafaa kiuchumi.
Kila
wanachoambiwa wanaona hawawezi.
Kila
wazo wanalopata wanaona hawawezi.
Hawawezi
biashara, hawawezi kufuga, hawawezi kulima hawawezi chochote.
Wanajiona
wana uwezo ama ujuzi mdogo kuliko wenginge.
Ukweli
ni kwamba ,
Unaweza kufanya karibu kila kitu ambacho ni cha kawaida kama tu
utaamua kujifunza.
Kila
kitu ambacho wapo watu wanaoweza , basi upo uwezekano wa wewe kuweza.
Tofauti
ya wale wanaoweza na wasioweza ilianza pale wale wanaoweza walipoamua kuweza na
wakaamua kujifunza.
Unaweza
hata kufanya upasuaji wa moyo kwa binadamu kama utaamua kujifunza. Wanaorusha ndege
nao kuna siku walikuwa kama mimi nawewe, sema tu waliamua kujifunza.
Wanaofanya
bishara kubwa kuna siku walikuwa kama mimi na wewe, sema tu kuna siku waliamua
kuweza na wakaanza kujifunza.
KIla unayemtamani uwezo wake naye aliwahi kuwa kama wewe.
HATA WEWE UNAWEZA, UKIAMUA KUWEZA

0 comments:
Post a Comment